Dk. Shika kutokea katika video mpya ya Dogo Janja?!
Kila siku umaarufu wa Dk.Luis Shika unazidi kuongezeka na hata baadhi ya watu na makampuni wameanza kumtumia katika biahara zao, hii ni pamoj na picha zilizoanza kusambaa zikimuonyesha yupo na msanii wa muziki Dogo Janja.
Kutokana na picha ambazo zimeanza na zinaendelea kusambaa mtandaoni zikimuonyesha Dk.Shika au Mzee wa 900 Itapendeza akiwa katika muonekano wa kipapa na huku akiwa ana kula bata na warembo, jambo linalohisiwa kuwa huwenda kukawa na video mpya ya muziki kutoka kwa msanii Dogo Janja hivyo ametumika kama muhusika mkuu.
Dk. Luis Shika amejipatia umaarufu kutokana na sakata la kuuzwa kwa nyumba za mfanyabiashara Said Lugumi, ambapo aliingilia kati kwa kutaja kiwango kikubwa cha pesa ili aweze kununua nyumba hizo, ila cha kushangaza baada ya kuibuka mshindi hakuwa na 25% za kumfanya aweze kuwa mmiliki halali wa nyumba hizo na ikapelekea kukamatwa na polisi na kumuweka rumande ambapo alitoka baada ya siku kadhaa na kuanza kupata umaarufu mara dufu.
No comments